Majambazi Yaua Polisi 3 Mbagala, Dar

ASKARI polisi watatu wameuawa kwa kupigwa na raisasi na majambazi huko Mbagala, Mmbande jijini Dar es Salaam usiku huu.
Inadaiwa kuwa askari hao walikuwa wakibadilishana lindo katika Benki ya CRDB, tawi la Mbagala Mmbande na mara wakaibuka watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi na kuanza kuwashambulia kwa risasi na baada ya shambulizi hilo wanadaiwa kuondoka na pikipiki wakielekea maeneo ya Mvuti.
Polisi waliouawa ni pamoja na;
E5761 CPL YAHAYA
F4660 CPL HATIBU
G9544 PC TTITO.
Inasemekana kuwa tukio hilo limetokea mnamo saa 1: 30 usiku katika na inadaiwa kuwa wahalifu hao waliondoka na silaha moja aina ya SMG.
Mmoja kati ya polisi waliouawa alikuwa anaingia lindo, mmoja alikuwa anatoka na mwingine alikuwa dereva na imeelezwa kuwa majambazi hayo hayakuingia ndani ya benki ila gari la polisi (Leyland Ashok) limeharibiwa  kwa risasi.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo: “Ni kweli kumetokea tukio la uvamizi hapa Mbagala lakini taarifa kamili nitazitoa kesho kwa kuwa bado nipo eneo la tukio kwa ajili ya uchunguzi zaidi”. Alisema Kamanda Sirro.

No comments

Powered by Blogger.