Hukumu Kesi ya Babu Tale Yaahirishwa Tena

HUKUMU ya kesi inayomkabili Meneja wa Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, Babu Tale, ya kusambaza na kuuza DVD za mawaidha ya Shehe Hamis Mbonde bila ridhaa yake imeahirishwa tena leo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam mpaka Septemba 12, mwaka huu.
                                                               babu tale na diamond
Kwa mujibu wa Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mustapha Sian alisema sababu kubwa ya kuahirishwa kwa kesi hiyo ni kwamba aliyetakiwa kuitolea hukumu ambaye ni Msajili Projest Kahyoza hayupo mahakamani kikazi.
Katika kesi hii Babu Tale, pamoja na mdogo wake anayeunda kundi la Tip Top Connection wanatakiwa kuieleza mahakama kwa nini wasifungwe jela ama kumlipa Shehe Mbonde kiasi cha Sh. Milioni 250.

No comments

Powered by Blogger.