IDARA YA UHAMIAJI:MGOMBEA URAIS WA TFF WALLACE KARIA NI RAIA HALALI WA TANZANIA

                                    
                                                      Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanga

Idara ya Uhamiaji Nchini imethibitisha kuwa  Kaimu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Wallace John Karia ambaye ni Mgombea Urais wa TFF  katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika August 12  mwaka huu ni Raia halali wa Tanzania.

Akizungumza na waandishi habari makao makuu ya Idara hiyo, Msemaji Mkuu wa Uhamiaji,  Ally Mtanga amesema kuwa mmoja wa wagombea wa Urais wa TFF alimkatia rufaa mgombea mwenzake Wallace Karia kuwa si raia wa Tanzania  hali ambayo inafanya akose sifa ya kuwa mgombea wa kiti hicho.

"Wallace Karia ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa chini ya kifungu cha 5(1) na (2) cha sheria ya uraia ya Tanzania sura ya 357(Rejeo la 2002) na kanuni zake, wakati huo huo akiwa raia wa Somalia kwa kurithi".

Mtanga amesisitiza  utambuzi wa uraia upo kisheria sura ya 357 (rejeo la 2002} uraia hauangaliwi Rangi, kabila wala dini.

Idara hiyo imevitaka vilabu vyote na taasisi za michezo kuhakikisha wafanyakazi wote na wachezaji ambao raia wa kigeni wanatimiza taratibu zote za kisheria za kukaa nchini  bila kufanya hivyo sheria itashika mkondo wake .

No comments

Powered by Blogger.