IGP SIRRO AKUTANA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOANI MWANZA

 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro (katikati), akimsikiliza Mkuu wa mkoa wa
Mwanza, John Mongella, wakati alipofika ofisini kwake jana. IGP Sirro, yupo mkoani humo
ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi, yenye lengo la kujitambulisha kwenye Kamati ya
Ulinzi na Usalama pamoja na kuzungumza na askari wa Jeshi hilo. kulia ni Kamanda wa Polisi
mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi, DCP Ahmed Msangi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro (aliyesimama), akizungumza na baadhi ya
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Mwanza, kwa lengo la kujitambulisha, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la
kuzungumza na askari wa Jeshi hilo.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Mwanza, alipofika kwa lengo la kujitambulisha, ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la
kuzungumza na askari wa Jeshi hilo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya askari wa Jeshi hilo baada ya kumaliza kikao kazi na maofisa na askari ambapo aliwasisitiza kuzingatia weledi wakati wa kutekeleza majukumu yao. Picha na Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi.

No comments

Powered by Blogger.