HULL CITY YAIBANA MBAVU MANCHESTER UNITED OLD TRAFFORD

 Kipa Eldin Jakupovic ameokoa magoli kadhaa wakati Hull City ikiichanganya Manchester United kwa kufanikiwa kutoka sare tasa katika mchezo wa Ligi Kuu kwenye dimba la Old Trafford.

Wenyeji Manchester United walishinda kabisa kupata ujanja wa kutumbukiza mpira kumpita kipa wa Hull, ambaye alizuia kiufundi shuti la mbali la Zlatan Ibrahimovic na jitihada za shambulizi la Paul Pogba katika kipindi cha kwanza.

Kwa matokeo hayo Manchester United wanabakia katika nafasi ya sita, lakini yameisaidia Hull City kujikwamua kutoka chini kwenye msimamo.
            Zlatan Ibrahimovic akijipinda kuachia shuti akijaribu kutafuta goli
                        Marcus Rashford akijaribu bila ya mafanikio kulenga goli

No comments

Powered by Blogger.