GABRIEL JESUS AFUNGA GOLI WAKATI MAN CITY IKIUA

Mchezaji Gabriel Jesus amefunga goli lake la kwanza akiwa na Manchester City wakati wakiichakaza West Ham 4-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza katika dimba la London.

Manchester City, ambao walimuacha mshambuliaji wa Sergio Aguero na kipa Claudio Bravo akiwa benchi walipata goli la kuongoza kupitia kwa Kevin de Bruyne baada ya kugongeana vyema na Jesus.

Dakika nne baadaye Leroy Sane aliwapita mabeki wawili na krosi yake iliyobabatizwa ikamkuta David Silva na kufunga goli. Raheeem Sterling alimtengenezea goli Jesus na Yaya Toure akafunga goli la nne kwa mkwaju wa penati katika kipindi cha pili.
                     Kevin de Bruyne akifunga goli la kwanza la Manchester City
                            Yaya Toure akipiga mkwaju wa penati na kufunga goli

No comments

Powered by Blogger.