KOCHA ARSENAL ARSENE WENGER KUTOSOMA KITABU CHA HASIMU WAKE JOSE MOURINHO


Kocha Arsenal, Arsene Wenger, amesema hatosoma kitabu cha kocha mwenzake wa Manchester United, Jose Mourinho, ambacho amenukuliwa akisema atauvunja uso wa kocha huyo Mfaransa.

Jose Mourinho amekuwa mara kwa mara akigombana na Wenger wakati alipokuwa na Chelsea, na aliwahi kumueleza Wenger kuwa atakuja kuwa mtu spesho wa baadaye.

Alipoulizwa iwapo atasoma kitabu hicho Wenger amesema hayupo katika muda wa kuharibu, kwani kwa sasa anatilia mkazo kujiimarisha na mchezo wao wa jumamosi dhidi ya Chelsea.

Mourinho, 53, aliwahi pia kumuelezea Wenger sawa na mla chabo (kozi), mwaka 2005 baada ya Mfaransa huyo kuhoji sera za uhamisho wa Chelsea.
        Arsene Wenger na Jose Mourinho wakitaka kuzidunda kavu kavu

No comments

Powered by Blogger.