NEWS ALERT: RAIS KIKWETE AFANYIWA UPASUAJI WA TEZI DUME MAREKANI, HALI YAKE INAENDELEA VYEMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho 

Kikwete alfajiri ya jana, Jumamosi, Novemba 8, 2014, alifanyiwa

upasuaji wa tezi dume (prostrate) katika Hospitali ya Johns Hopkins

iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.

 Rais Kikwete amefanyiwa upasuaji huo baada ya madaktari waliomfanyia

uchunguzi wa afya yake kujiridhisha kuwa Rais alikuwa anahitaji

matibabu ya aina hiyo.

 Upasuaji huo uliofanyika alfajiri na kuchukua kiasi cha saa moja

unusu, umefanyika salama na kwa mafanikio makubwa.

Hali ya Mheshimiwa

Rais Kikwete inaendelea vizuri, bado yuko wodini akiendelea kuwa chini

ya uangalizi wa madaktari na kupatiwa tiba.

 Wananchi wataendelea kupewa taarifa sahihi kuhusu hali ya Rais Kikwete

kwa kadri zitakavyokuwa zinapatikana.

 Imetolewa na

 KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS,

 IKULU DAR ES SALAAM,

NOVEMBA 9, 2014




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na  Dkt.Edward Shaeffer wa  hospitali ya Johns Hopkins (kushoto) na Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi  (kulia) muda mfupi baada ya kuwasili ili kufanyiwa upasuaji katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland Marekani Jumamosi asubuhi.Upasuaji huo uliochukua muda wa saa moja na nusu ulifanyika salama.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na daktari Bingwa Mpasuaji Edward Shaeffer muda mfupi kabla ya kuingia kwenye chumba cha upasuaji uliofanyika katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland nchini Marekani Jumamosi asubuhi(picha na Freddy Maro)

No comments

Powered by Blogger.