WANAOKWENDA KUSOMA VYUO VYA NGA'MBO LAZIMA WAWE NA VIBALI VYA TCU

 Mkuruegenzi  Mtendaji wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel
akizungumza  na Wanafunzi  wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya  nje ya nchi  wakiwa na wazazi wakipata taarifa juu taarifa mbalimbali kabla ya safari ya kwenda katika vyuo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Zamani wa Elimu, Mbunge wa Bagamoyo, Mhandisi Dk. Shukuru Kawambwa akizungumza na wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya nje katika Mkutano ulioandaliwa na Global Education Link (GEL) 
 Afisa wa Habari Mwandamizi wa Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU),Edward Mkaku akizungumza juu ya Global inavyofanya  kazi kwa ukaribu  na TCU kwa wanafuzi wanaokwenda  kuwa taarifa za  tume hiyo.
 Mwanasaikolojia ,Chris Mauki akizungumza juu ya masuala ya Saikolojia katika kuwajenga wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya nje ya nchi.
Baadhi ya wazazi wakichangia maada zinazohusiana na wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya Nje ya Nchi.


Wanafunzi wote wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya nje wametakiwa  kuwa na kibali cha Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) bila kufanya hivyo wanafunzi hao hawatatambulika kutokana na viwango walivyoweka.

Hayo ameyasema Afisa Habari Mwandamizi wa TCU, Edward Mkaku katika Mkutano wa Wanafunzi wanaokwenda kusoma Vyuo Vikuu vya Nje ya Nchi uliokuwa umeandaliwa na Global Link Education Link (GEL), kwa ajili ya kupeana maelekezo kwa Wanafunzi wanaokwenda nje kusoma vyuo Vikuu vya Nje ya Nchi mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Mkaku amesema GEL inafuata taratibu na huwa haipeleki wanafunzi vilaza ambao hawapati vibali kutotaka TCU. Amesema kuwa TCU ndio inafanya utambuzi wa vyuo ambavyo wanafunzi wanakwenda kusoma ikiwa ni kuangalia ubora wa vyuo hivyo.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa GEL , Abdulmalik Mollel amesema kuwa katika vitu wanavyofanya ni uhakika kwa wanafunzi kwenda kusoma katika vyuo vikuu vya nje ya nchi.Amesema mkutano huo wanaoufanya ni kujiweka wazi kuwa hakuna kificho kwa kile ambacho wanakifanya kwa wanafunzi wanaokwenda vyuo vikuu vya nje.

Waziri zamani wa Elimu , Sayansi na Teknolojia, Mbunge wa Bagamoyo, Mhandisi Dk. Shukuru Kawambwa amesema kuwa wanafunzi wakasome na kuweza kuleta maendeleo.

Amesema kuwa wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya nje wakapepelushe bendera kwa kufanya vizuri na kuweza kurudi vyeti.

No comments

Powered by Blogger.