TRA, Wajapani waipiga jeki Majimaji Selebuka 2017


 Wanafunzi wa Shule ya De Paul wakipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (Jica) kwa kuibuka kinara katika mdahalo kwenye Tamasha la Majimaji Selebuka.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya De Paul wakitabasamu na tuzo zao ya IPad na kikombe cha fedha kwa kushika nafasi ya pili katika mdahalo kwa shule za sekondari ulioandaliwa na Tamasha la Majimaji Selebuka 2017, 
 Nathan Mpangala akimtunuku mwanafunzi, Lucy Chenji wa Shule ya Sekondari ya Songea Girls wa kuibuka kinara wa shindano la uchoraji vibonzo. 

 Washindi wa mdahalo kwa shule za sekondari katika Tamasha la Majimaji Selebuka 2017, wakiwa na tuzo zao kwenye picha ya pamoja na majaji wa mdahalo huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Manispaa ya Songea. 
 Wawili kutoka kushoto ni wanafunzi wa Songea Girls iliyoshika nafasi ya pili, bingwa Shule ya De Paul na Chipole iliyoshika nafasi ya tatu.
 Mwakilishi wa shule Iliyoshika nafasi ya pili katika mdahalo sekondari ya Songea Girls akipokea tuzo ya kikombe cha fedha kutoka kwa Mjumbe Wa Kamati ya Tamasha la Majimaji Selebuka, Hilary Ndumbaro kwa kuwa ya pili katika mdahalo kwa shule za sekondari.
  Mwanafunzi Magreth Gama wa shule Songea Girls, akipongezwa na mwakilishi wa Jica, Emmanuel Masalu kwa kuibuka kinara wa uwasilishaji bora (best presenter) kwenye mdahalo kwa shule za sekondari

Sehemu ya wanafunzi kwenye mdahalo huo, wenye mada ya “Ulipaji wa kodi hauepukiki kwa tija ya maendeleo ya nchi yetu.”


Na  Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeongoza washirika wengine kama Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (Jica) na Chuo Kikuu Huria Tanzania (Open) kulipiga jeki tamasha la kila mwaka la Majimaji Selebuka kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa shule zilizofanya vema katika shindano la mdahalo kwa shule za sekondari uliofanyika siku mbili kabla ya kupata washindi.
Jumla ya shule za sekondari 12 za awali (O-Level) na upili (A-Level), zilichuana vikali katika mdahalo huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Manispaa ya Songea na kushuhudia Shule ya Sekondari ya De Paul ikiibuka kidedea kwa kupata alama 42.6 na kutetea taji lao la mwaka jana, ikizibwaga shule za Songea Girls (alama 41.6) na Chipole/St Agness (41.2) zilizoshika nafasi ya pili na tatu, huku Kigonsela wakishika nafasi ya nne na alama zao 41.1.
Aidha, katika kutia motisha na hamasa kwa tija ya maendeleo ya elimu mashuleni, TRA waliwatunuku washindi kitita cha fedha laki mbili kwa bingwa na mshindi wa pili 150,000, mshindi wa tatu 100,000 na wa nne 50,000 huku walimu waliombatana nao wakila 50,000.
TRA katika kile kilichotafsiriwa kuvutiwa na mada iliyojadiliwa ya ‘Ulipaji Kodi hauepukiki kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu’ walikwenda mbali na kuwatuza wawasilishaji bora na fanisi (best presenter) ambapo Magreth Gama wa Songea Girls aliibuka kinara na kukunja 150,000. Nafasi ya pili ilichukuliwa na Sebastino Lubinda (Kigonsela, 100,000) na Monica Shilima wa De Paul aliyeshika nafasi ya tatu na kuondoka na 50,000.
Nalo shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) walitoa zawadi IPad kwa shule tatu zilizoshinda. IPad hizo zina notice za masomo yote kuanzia kidato cha kwanza hadi ya sita. Aidha, Chuo Huria Tanzania (Open) kimetoa zawadi ya fulani kwa shule zilizofanikiwa kuingia kwenye mchujo wa mwisho.
Wachoraji Bora
Katika kuhimiza maendeleo shuleni, Balozi wa Tamasha la Majimaji Selebuka, Nathan Mpangala kupitia Jukwaa la Mtukwao aliandaa shidano la uchoraji vibonzo vyenye ujumbe wenye kuvuti na nafasi hiyo imechukuliwa na mwanafunzi wa Songea Girls, Lucy Chenji akifuatiwa na Husna Omar na Wilbard Joseph katika nafasi ya pili na tatu.
SHULE ZILIZOSHIRIKI:
De Paul, Songea Girls, Chipole/St Agness, Kigonsela (zilizofika nusu fainali). Nyingine ni Agustivo, Dr Emmanuel Nchimbi High School, Mfaranyaki, Bombambili, Mashujaa, Msamala, Londoni na  Ruvuma

No comments

Powered by Blogger.