Picha: Zari atua hospitali kumjulia hali ex wake Ivan

                                      Zari akiwa hospital kumjulia hali ex wake
Mama watoto wa Diamond, Zari the Bosslady ameonekana katika picha akimjulia hali ex wake Ivan Ssemwanga ambaye anadaiwa kulazwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini baada ya kupata matatizo ya moyo.
Ivan ambaye alipata watoto watatu na Zari, anadaiwa kukimbizwa hospitali wiki hii baada ya kupoteza fahamu.
Jumatatu hii Zari alipost picha ya mshumaha na kuwaomba mashabiki wake kumuombea mzazi mwenzake huyo.
Hapo jana Zari kupitia ukurasa wake wa SnapChat aliandika “Siku mbili kwangu zimekuwa ngumu, nawaomba tumuombee Ivan”.
Mitandao ya Uganda inadai kuwa Ivan anasumbuliwa na maradhi ya Shambulio la Moyo (Coronary Artery Disease).
chanzo bongo5

No comments

Powered by Blogger.