Mnawatumia wasanii kama makarai - Prof Jay
Mbunge wa Mikumi. Mh. Joseph Haule akiwa na Mbunge wa Jimbo la Mbeya
Mjini, Joseph Mbilinyi bungeni katika moja ya kikao cha Bunge
kilichopita.
Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Joseph Haule amefunguka na kuitaka serikali kuwekeza fedha za kutosha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili wizara hiyo iweze kuwekeza katika sanaa na kuacha kuwatumia wasanii kama makarai ya kujengea.
Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Joseph Haule amefunguka na kuitaka serikali kuwekeza fedha za kutosha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili wizara hiyo iweze kuwekeza katika sanaa na kuacha kuwatumia wasanii kama makarai ya kujengea.
Prof Jay alisema hayo leo Bungeni wakati akichangia makadilio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari kwa mwaka 2017/ 2018
credit .eatv
"Wasanii wa Tanzania
wamekuwa katika mazingira magumu sana na wamekuwa katika umasikini
mkubwa licha ya mara nyingi kutumiwa katika kampeni mbambali na hata
katika chaguzi zilizopita mmeona jinsi wasanii walivyokuwa wakitumika,
mmewatumia kama makarai na baada ya hapo mmeyaweka uvunguni, tunajua
makarai huwa yanatumika kwenye kujenga maghorofa na vitu vingine lakini
nyumba ikikamilika yanawekwa uvunguni hayatakiwa kuonekana hata kwa
wageni" alisema Prof Jay
Mbali na hilo Prof Jay amesema wasanii wengi wa Tanzania wanakuwa
masikini sana sababu wakishatumika huwa hawathaminiwa tena na kuachwa
mpaka wakati mwingine wa uchaguzi au kampeni credit .eatv
Post a Comment