Mnawatumia wasanii kama makarai - Prof Jay

Mbunge wa Mikumi. Mh. Joseph Haule akiwa na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi bungeni katika moja ya kikao cha Bunge kilichopita.

Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Joseph Haule amefunguka na kuitaka serikali kuwekeza fedha za kutosha katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili wizara hiyo iweze kuwekeza katika sanaa na kuacha kuwatumia wasanii kama makarai ya kujengea.
Prof Jay alisema hayo leo Bungeni wakati akichangia makadilio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari kwa mwaka 2017/ 2018 
"Wasanii wa Tanzania wamekuwa katika mazingira magumu sana na wamekuwa katika umasikini mkubwa licha ya mara nyingi kutumiwa katika kampeni mbambali na hata katika chaguzi zilizopita mmeona jinsi wasanii walivyokuwa wakitumika, mmewatumia kama makarai na baada ya hapo mmeyaweka uvunguni, tunajua makarai huwa yanatumika kwenye kujenga maghorofa na vitu vingine lakini nyumba ikikamilika yanawekwa uvunguni hayatakiwa kuonekana hata kwa wageni" alisema Prof Jay 
Mbali na hilo Prof Jay amesema wasanii wengi wa Tanzania wanakuwa masikini sana sababu wakishatumika huwa hawathaminiwa tena na kuachwa mpaka wakati mwingine wa uchaguzi au kampeni 
credit .eatv

No comments

Powered by Blogger.