Hizi ni Sentensi 32 Za Diamond Platnumz Alipohojiwa na Clouds FM, Amfungukia Wema
Hizindizo sentesi 32 alizoongea mkali wa
Bongo fleva hapa nchini, Diamond platinums jana alipojiwa jana Novemba
23, 2016 kwenye Kipindi cha XXL cha Clauds FM ya jijini Dar es Salaam.
#Diamond_: Mwanamuziki hutakiwi kufanya
haraka kwenda Marekani, kwanza jipigie promo kisha utakwenda, na
kuthaminika utathaminika.
#Diamond_: Wimbo na Neyo haukuvuja bali
upo katika promosheni chini ya Univeral Studio ambao niliingia nao
mkataba na kunilipa dola milioni moja (Shilingi bilioni mbili),
waliandaa dola laki tano, nikakaza, wakaongeza, na hawakunichukua mimi
tu, niliwaambia wachukue Lebo nzima ya Wasafi, wakafanya hivyo.
#Diamond_: Universal ni kampuni kubwa,
imewahi kuwasimamia wanamuziki wengi, Akon, Bob Marley, Lady Gaga,
Justine Bieber, Nicki Minaj, hata hii ngoma ya Drake ipo chini yao, kwa
kifupi ukiwa na hawa washikaji, utatangazwa sana duniani.
#Diamond_: Nilikutana na Roc Nation,
wakataka kunisaini, nilikataa kwanza, tuliporudi, Universal wakanipigia
simu na kulalamika kwamba inakuwaje nitake kusaini na Roc na wakati wao
walianza? Wakaniambia nichukue ndege, nikaenda South kukutana nao.
#Diamond_: Mkataba na Universal
hauhusiani na shoo kwamba kiasi kikiingia kwenye shoo wachukue, hapa,
hiyo ni kwenye mauzo ya kazi zetu tu duniani.
#Diamond_: Wasanii wengine wanaingia
mikataba na kampuni nyingine kuwa, wanashuka kwa sababu mikataba yao si
mizuri, hawana wasimamizi wazuri, wao wanachoangalia ni sifa za
kusainiwa na kampuni kubwa bila kujali watapata nini, mikataba itawabana
vipi.
#Diamond_: Huwezi kununua viewers kwenye
Youtube, nyimbo zangu kwa mwaka huu zimekuwa na viewers wengi na ndiyo
maana nikapewa tuzo, si mimi tu, hata Millard Ayo amepewa, je, hii
inamaanisha naye Millard amenunua tuzo?
#Diamond_: Nilitakiwa kufanya shoo Kongo ila tuliiacha kwa sababu kuna vitu hawakuelewana na menejimenti yangu.
#Diamond_: Universal wanataka kuniingiza
kwenye soko la kidunia na ndiyo maana wakaanzisha tour yangu na Neyo
nchini Uingereza, hii yote ni kunitangaza.
#Diamond_: Huko nitakutana na Wazungu,
asilimia ndogo watakuwa watu weusi. Sasa mtu akiniona, atasema ndiye
huyu bwana ambaye tuliusikia wimbo wake, mwisho wa siku wanatazama video
zako na viewers kufika milioni 50…hapo ndo watasema nimenunua kabisa.
#Diamond_: Muziki si ushirikina, ni mipango na subira, hutakiwi kuwa na haraka.
#Diamond_: Mimi ni mwanamuziki pekee niliyelipa kodi shilingi milioni 35, siyo useme una maendeleo halafu hulipi kodi.
#Diamond_: Mimi ni mwanamuziki pekee mwenye nyumba South Africa
#Diamond_: Mimi ni mwanamuziki pekee
ninayepiga shoo hata nchi za mbali. Wengine wanaishia Kenya tu, mtu
anakwenda Rwanda, anapiga shoo hata kuonyesha tuone haonyeshi.
#Diamond_: Rwanda nilipiga shoo uwanja
mzima ukajaza. Wakaniambia mtu ambaye aliwahi kujaza uwanja namna hiyo,
mara ya mwisho alikuwa Lucky Dube, baada ya hapo, hakukuwa na mwingine
zaidi yangu.
#Diamond_: Unaweza kuwa na sauti, bila kujua unatunga kitu gani utaonekana kama unapiga kelele.
#Diamond_: Muziki ungekuwa ni sauti ningemsaini Wema Sepetu.
#Diamond_: Mwanamuziki anasema muziki
wangu ni wa ujanjaujanja, kama wangu wa ujanjaujanja mbona unavuma mpaka
nje halafu wako hauvumi unaishia hapahapa Tanzania?
#Diamond_: Mwanamuziki mkali ni yule
ambaye hata muziki wake unavuma Afrika nzima. Sasa huna hata weimbo
unaovuma Afrika nzima, ukali wako upo wapi?Huna shoo, shoo zako nyingi
Tanzania, ukipata Kenya basi mshikaji wako kakuunganisha.
#Diamond_: Kuna caption nilitaka kupost
jana isemayo “Tatizo wanatumia nguvu nyingi kwenye makoo pasipo kutumia
akili ndo maana muziki wao unaishia Chalinze”
#Diamond_: Sipendi kuongea, ukiona nimeongea basi jua kuna vitu vinaendelea, watu wanapiga majungu.
#Diamond_: Watu wanaosema ni wakali, nishaomba kolabo, wamenikimbia.
#Diamond_: Niliomba nifanye shoo nao uwanja wa taifa ya nani mkali, wamekataa.
#Diamond_: Niliongea na Makamba
atudhamini, tufanye shoo hiyo ya mkali nani lakini wao wanakimbia,
hawataki, sasa ukali wao upo wapi? Kama wewe mkali, kwa nini unakimbia?
#Diamond_: Watu wanaona tukimdiss
Diamond ni kiki, busta, mimi sasa hivi nawakaribisha, ili busta walipate
vizuri, tufanye mkali nani.
#Diamond_: Nilifanya nao shoo na CCM,
hawakuposti shoo zao. Tena nilichokuwa nafanya, mtu anapafomu, mimi
nashuka chini, shoo yote inakufa.
#Diamond_: Kama shoo unaogopa, tufanye
hata wimbo. Nakupa beat ukae nayo hata mwaka mzima, halafu mimi siku
moja tu, halafu ndiyo nitakuonyeshea mimi nani.
#Diamond_: Mimi ni mwanamuziki mstarabu japokuwa image yangu inaonekana kama mvuta bangi, mimi si mtu wa wanawake.
#Diamond_: Kama unajiamini tupige shoo, sitokupeleka Zimbabwe kwa sababu hujulikani, tupige hapahapa Tanzania.
#Diamond_: Dimpoz kashatuma watu wengi
kuomba msamaha, kashamtuma Salam. Alishanipigia mpaka simu, sikupokea,
sasa ningezungumza nini?
#Diamond_: Mimi sina matatizo na watu bali watu wana matatizo na mimi na ndiyo maana watu wakiweka matatizo na mimi wanafeli.
#Diamond_: Wengine wanasema mimi mshirikina, sivai pete ya kijani, navaa gold, navaa silva, sina majini kwenye mkono wangu.
Post a Comment