MKUU WA MKOA WA ARUSHA ATOFAUTIANA NA MBUNGE LEMA KATIKA UZINDUZI WA UJENZI WA HOSPITALI YA MAMA NA MTOTO

 Picha ikionyesha wa kushoto mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwa anatulizwa na mchungaji Wilfred Mlayi, na kulia ni mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwa anatulizwa na mfadhili wa Mradi huo ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya kina mama na mtoto duniani Edru Broun
Mwananchi aliyehudhuria uzinduzi wa ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto ambaye hakupenda kutaja jina lake akiwa anamuomba Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kutulia na kumuaacha mkuu wa mkoa aendelee kutoa hutuba
 
                                                                          
Habari picha na Woinde Shizza, Arusha
 
VURUGU kubwa zimeibuka baina ya mkuu wa mkuu wa mkoa Arusha Mrisho Gambo na mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Burka nje kidogo ya jiji la Arusha.

Vurugu hiyo zimeibuka baada ya mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuvuruga ratiba iliyokuwa imepagwa na waandaaji wa hafla hiyo, ambapo kwa mujibu wa ratiba iyo ilikuwa imepagwa kuwa hotuba ya mkuu wa mkoa ingetanguliwa na waandaji wa shughuli hiyo akiwemo waandaji wa hafla hiyo,wafadhili pamoja na mbunge Lema.

Kabla ya vurugu hizo mkuu wa Arusha alikaribishwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Alexzanda Mnyeti swala ambalo liliibua mzozo mkubwa kwa wananchi walikuwa wamefika kushuudia tukio hilo la uzinduzi wakiwemo wafadhili waliofadhili mradi ambao ni shirika la kuhudumia afya ya mama na mtoto (maternity Afrika ).

Baada ya kuanza kuhutubia mkuu huyo wa mkoa akielezea historia ya mradi huo ikiwa upatikanaji wa eneo la kujenga mradi wa hospitali hiyo gafla mbunge Lema alipo simama na kupinga hotuba hiyo na kudai imejaa upotoshwaji na siasa ndani kwani yeye ndie aliyetafuta eneo hilo la ujenzi wa hospitali hiyo kutoka kampuni ya Mawala Advocate na sio kweli eneo hilo limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate Nyaga Mawala ya mda mrefu .

 
“mkuu wa mkoa acha kupotosha umma ,mchungaji simamisha hutuba ya mkuu wa mkoa imejaa siasa anaongea uongo anaongea vitu asivyo vijua,sitakubali huu uongo uendee siwezi kubali hutuba iendelee kwani anaongea uongo ,akitaka atumie nguvu ya polisi siogopi kufa ila nataka ukweli ,na aondoe siasa aseme ukweli hili jamboni la maendeleo ya wananchi na ni kwa faida ya wananchi haswa mama na mtoto tena wale wasio jiweza kwa hiyo naomba mkuu wa mkoa acha uongo”alisikika Lema akisema kwa sauti kubwa huku akimsogelea mkuu huyo wa mkoa.

Jambo hilo liliwalazimu baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo wakinamama kumpigia magoti mbunge huyo alionekana akiwa na jazba kubwa huku akimsogelea mkuu huyo wa mkoa swala ambalo lingeweza kusabisha uvunjifu wa amani .

Licha ya Vurugu hizo na kelele za wananchi walionekana nao kupinga hotuba hiyo ya mkuu wa mkoa,Mkuu wa mkoa wa Arusha aliendelea kuhutubia akiwa anaeleza kuwa eneo hilo lilitolewa na marehemu Nyaga Mawala kwa serikali ili liendelezwe kwa kujengwa hospitali na mama na mtoto kitendo ambacho kiliendeleza kelele za wananchi zikipinga hotuba hiyo wakidai mkuu wa mkoa anapotosha .
 
“hili jambo sio la siasa tusiingize siasa ,na kama kuna mtu ana mpango wa kufanya siasa apa anapoteza muda wake mimi ni mkuu wa mkoa na ninafahamu historia ya eneo hili”alisema Gambo

Kwa upande wake mfadhili wa maradi huo ambaye ni daktari bingwa wa magonjwa ya Festula Duniani Dkt.Edru Broun alieza kusikitishwa na tukio lilijitokeza na kuwataka viongozi waweke pembeni siasa zao na tofauti zao na wamtangulize mungu ili kutimiza shabaha ya ujenzi wakituo hicho cha hospitali kitakachoweza kumsaidi mama na mtoto.
 
Alisema kuwa ujenzi wa hopitali hiyo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni sita na kwa awamu ya kwanza kiasi cha shili bilioni tatu kitatumika kujenga hospitali hiyo fedha ambazo zitatolewa na wafadhili kutoka shirika la mama na mtoto (martenity Afrika).

Kwa upande wake mwenyekit wa Tasisi ya maendeleo ya jiji la Arusha (ARDF) Elifuraha Mtowe Alisema kuwa eneo la kujengwa hospitali hiyo lilitolewa na marehemu Nyaga Mawala na kwa ARDF kupitia ofisi ya mbunge wa jimbo la Arusha mjini ndipo taasisi yao ya ARDF ikaamua kutafuta mfadhili ndipo walipompata MartenityAfrika.

Alisema kuwa tangu wampate mfadhili waliingia mkataba na wakakubaliana hospitali iishe ndani ya mika mitano lakini mfadhili mwenyewe aliwaakikishia kuwa hospitali hiyo itaisha mapema  kwani itakamilika ndani ya mwaka mmoja tu ili mama na mtoto aweze kupata huduma kwa araka zaidi.

Awali mbunge Lema aliwaambia waandishi wa habari kuwa mkuu wa mkoa huyo alikuwa amegoma kuja kuzindua hospitali hiyo hadi pale mbunge huyo alipoamua kumpiga simu katibu mkuu kiongozi John Kijazi na kumwambia kuwa mkuu wa mkoa kagoma kuja kuzindua hospitali hiyo ndipo katibu mkuu alipoamua kupiga simu wizara ya Tamisemi ambapo ndio walimpigia simu mkuu wa mkoa ili aweze kufika kwenye uzinduzi huo.

No comments

Powered by Blogger.