THEO WALCOTT AONYESHA MAKALI YAKE NA KUIPA USHINDI ARSENAL

Theo Walcott ameonyesha makali yake kwa kufunga magoli mawili wakati Arsenal ikiibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Basel katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Iliwachukua washika mitutu dakika sita kupata goli la kwanza kupitia Walcott akifunga kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Alexis Sanchez.

Wachezaji hao wawili wa Arsenal walishirikiana tena na kutoa fursa kwa Walcott kufunga goli la pili kwa shuti la chini.
                        Theo Walcott akifunga goli lake la kwanza kwa kichwa
                       Theo Walcott akianguka chini baada ya kutupia goli la pili

No comments

Powered by Blogger.