REAL MADRID YAITWANGA BARCA; RONALDO AKITOLEWA NJE KWA KADI

 Cristiano Ronaldo amefunga goli na kisha akatolewa nje kwa kadi nyekundu wakati Real Madrid ikiifunga Barcelona magoli 3-1 katika mchezo wa kwanza wa kombe la Super Cup.

Katika mchezo huo Gerard Pique alijikuta akijifunga kwa kutumbukiza mpira katika goli lao akijaribu kukoa krosi ya Marcelo kabla ya Lionel Messi kusawazisha kwa mkwaju wa penati.

Ronaldo, aliyetokea benchi alifunga goli la pili la Real Madrid baada ya kutoka mbio na mpira umbali wa nusu ya kiwanja.

Ronaldo alipewa kadi ya kwanza kwa kushangilia goli hilo kwa kuvua jezi na kisha baadaye akapewa kadi ya pili kwa kujiangusha, kabla ya Marco Asensio kufuga goli la tatu.
        Cristiano Ronaldo akishika kichwa asiamini baada ya refa kumpa kadi ya pili ya njano
                                   Gerard Pique akijifunga goli wakati akijaribu kuokoa mpira

No comments

Powered by Blogger.