MANCHESTER UNITED YAICHAPA WEST HAM, 4-0


                                                  Pogba na Lukaku wakipongezana.
 Straika wa Romelu Lukaku akishangilia baada ya kutupia dhidi ya West Ham United katika Ligi Kuu ya England ‘Premier League’.
                                           Paul Pogba akishangilia baada ya kutupia.
Straika wa Romelu Lukaku ameanza vizuri maisha ya Manchester United baada ya kuiongoza timu yake hiyo kupata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya West Ham United katika Ligi Kuu ya England ‘Premier League’.
Lulaku ambaye alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza wa Premier League akiwa na kikosi chake hicho kipya, alionyesha uwezo mzuri na kutupia mabao mawili hivyo kuwa na mwanzo mzuri.
Lukaku alifunga mabao yake katika dakika ya 33 na 52 wakati bao la tatu liliwekwa wavuni na Anthony Martial katika dakika ya 87 baada ya kuingia akitokea benchi pamoja na Paul Pogba dakika ya 89 ambapio alipiga shuti kali lilijaa wavuni kutoka nej ya eneo la 18.

No comments

Powered by Blogger.