YANGA YATANGAZA KUMSAJILI KIPA WA SERENGETI BOYS, ASAINI MIAKA MITANO

Baada ya tetesi ndani ya wiki kadhaa, hatimaye Klabu ya Yanga imetangaza kumsajili kipa chipukizi, Ramadhani Kabwili.
Kipa huyo aliyekuwa akiidakia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys amesaini mkataba wa miaka mitano kuitumikia klabu hiyo yenye makao makuu mitaa ya Jangwani jijini Dar es Salaam.
Kabwili anaungana na kipa mwingine mpya, Mcameroon Youthe Rostand aliyesajiliwa kutoka African Lyon na Benno Kakolanya ambaye huu utakuwa msimu wa pili tangu asajiliwe akitokea Tanzania Prisons ya Mbeya.
Kabwili na Rostand wote wanasajiliwa kuchukua nafasi za makipa wa muda mrefu wa Yanga, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Deogratius Munishi ‘Dida’ waliomaliza mikataba yao na kuruhusiwa kuondoka.

No comments

Powered by Blogger.