Mourinho amrudisha Zlatan United

Jose Mourinho yupo katika mazungumzo yakuona ni kwa namna gani Zlatan Ibrahimovic anaweza kurejea Manchester United
 Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho amemuambia mchezaji wake Zlatan Ibrahimovic kuwa milango bado ipo wazi kwa yeye kurejea kwaajili ya msimu ujao.Ibrahimovic  mwenye umri wa miaka 35 alipata majiraha ya kifundo cha mguu katika mchezo wa michuano ya Europa League dhidi ya timu ya Anderlecht uliochezwa mwezi Aprili na kufanikiwa kuchomoza na ushindi wa magoli 2-1.
             Ibrahimovic alipopata majeraha katika mchezo wao na  Anderlecht
Mchezaji huyo amefunga jumla ya magoli 28 tangu alipojiunga na United kwa mkataba wa mwaka mmoja ambao tayari umemalizika.
Mourinho amethibitisha kufanyika mazungumzo baina ya mchezaji huyo na uongozi na anatarajiwa kuonekana tena Old Trafod kipindi cha Christmas.

No comments

Powered by Blogger.