Nape: Niliunda kamati kuchunguza tukio la uvamizi, sio RC

                                                                      Nape Nnauye
 Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema kamati aliyounda ilikuwa kwa ajili ya kuchunguza tukio la uvamimizi wa Clouds Media na sio RC wa Dar es Salaam.Ukupitia mtandao wa twiter Nape ameandika,
‘Niliunda Kamati Kuchunguza tukio la kumamiwa kituo cha utangazaji sio kumchunguza RC. Kama RC alikuwa mmoja wa wavamizi, hayupo juu ya sheria!.Hiyo jana Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiwa Star Tv kwenye kipindi cha Tuongee Asubuhi alikana tuhuma zinazomkabali kuhusu uvamizi na kuongeza kuwa kamati iliyoundwa haikuwa na mamlaka ya kumuhoji.
“Sijawahi kuvamia kituo chochote kile cha runinga , nafasi yangu kama mkuu wa mkoa naweza kumuita mtu yoyote, nina maswali kama 50 kwenye lile neno ‘Kuvamia’ la kwanza wanasema nilivamia kipindi kirushwe wakati kipindi kile kilikuwa kiko live, Watanzania kama hapa tuko live hivi mtu unaweza kuvamia kweli wakati tuko live.” alieleza.

No comments

Powered by Blogger.