Video; Darassa apata ajali Kahama Mkoani Shinyanga...Jionee hapa




                                      Muonekano wa gari alilopata nalo ajali aina ya Toyota Harrier

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwanamuziki wa Hip Hop Bongo ambaye anasumbua na ngoma yake kali ya Muziki, Sharrif  Thabit ‘Darassa’ amenusurika kifo baada ya kupata ajali mbaya maeneo ya Ntobo barabara ya kuelekea Mgodi wa Bullyanhulu Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.
Habari zimeeleza kuwa ndani ya gari hilo aina ya Toyota Harrier  ambalo dereva hajajulikana, Darassa alikuwa ameambatana na director wake, Hanscana pamoja na producer wake, Abba Process na wote wametoka salama.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Darassa amethibitisha kupata ajali hiyo.

No comments

Powered by Blogger.