Video: Majonzi yamfanya mke wa Papa Wemba ashindwe kuzungumza kwenye tuzo za Afrima

Kwenye tuzo za Afrima 2016 zilizotolewa Jumapili, jijini Lagos, Nigeria, marehemu Papa Wemba ni miongoni mwa wasanii nguli wa Afrika waliopewa tuzo ya heshima. Kupokea tuzo hiyo, alikuwepo mke wake pamoja na mwanae wa kike. Hata hivyo mjane huyo alishindwa kabisa kuongea chochote kutokana na kuwa na huzuni kubwa. Bintiye alimwakilisha na kushukuru kwa upendo mkubwa kutoka kwa Waafrika tangu kifo chake. Alidai kuwa wamejiwekea nadhiri kumuenzi Papa Wemba kila siku katika maisha yao. Mwanae huyo pia alitumia fursa hiyo kuimba wimbo wa baba yake.

No comments

Powered by Blogger.