Witness asema kuwa moja ya mbinu za kupunguza uzito ni kufanya mapenzi angalau mara 3 kwa week!

Rapa wa kike Bongo, Witness a.k.a Kibonge mwepesi amesema kuwa moja ya mbinu za kupunguza uzito ni kufanya mapenzi angalau mara 3 kwa wiki au mara 18 kwa mwezi au hata zaidi ya hapo.
Witness ambaye anatoa huduma na elimu ya kusaidia kupambana na unene kupita kiasi amekaririwa na Planet Bongo ya EA Radio akisema kufanya mapenzi ni mbinu nzuri.
Witness amekuwa akifanya mazoezi kama njia moja ya kuzuia kunenepa na kufuata utaratibu mzuri wa ulaji wa chakula jambo ambalo amekuwa akiwashauri pia wateja wake lakini haijafahamika kuhusu hili la kufanya mapenzi kama analifanya pia.
Labda kwasababu ni jambo la faragha.

Mbinu nyingine aliyoitoa ni pamoja na kuepuka kula chakula cha usiku baada ya saa 3 usiku ili kuupa mwili muda mzuri wa kufanya mmeng’enyo kabla ya kulala.

No comments

Powered by Blogger.