Tambwe Awachimba Mkwara Mavugo, Bocco

MFUNGAJI bora wa msimu uliopita, Amissi Tambwe (pichani) amewachimba mkwara washambuliaji wa Simba, Laudit Mvugo na John Bocco wa Azam FC kwa kusema kuwa wasitarajie kutwaa tuzo hiyo msimu huu.
Tambwe aliibuka na ufungaji bora kwa kufunga jumla ya mabao 21 akifuatiwa na Hamis Kiiza aliyekuwa Simba ambaye na yeye alikuwa akikifukuzia kiatu hicho kwa kufunga mabao 19.
Akizungumza na tovuti hii, Tambwe ameeleza kuwa, lengo lake kubwa ni kuona anatetea kiatu chake hicho kwa kuonyesha ujuzi zaidi katika kufumania nyavu na kudai kuwa anaamini Mungu atamsaidia na kufanikisha lengo lake.
“Ligi inaonekana itakuwa ngumu kutokana na kila upande kujifua kikamilifu kuona unafanya vizuri na kwa upande wetu tumejiandaa pia kufanya vyema.

No comments

Powered by Blogger.