BANDARI WAPEWA MIEZI MITATU UJENZI FLOWMETER

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, alipofanya ziara ya kikazi bandarini hapo, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (kushoto), akitoa maelekezo kwa Mkururgenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko wakati akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka hiyo wakati alipofanya ziara ya kikazi, jijini Dar es Salaam. 
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Meli kutoka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Kapteni Abdullah Mwingano, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (wa tatu kushoto), kuhusu utaratibu wa upakuaji wa mafuta bandarini wakati alipofanya ziara ya kikazi katika Bandari ya Dar es Salaam.

Meneja Msaidizi wa Mifumo ya ukaguzi wa mizigo (Scanner), Bandari ya Dar es Salaam Bw. Jackson Paul, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, namna mifumo hiyo inavyofanya kazi wakati wa ziara yake ya kikazi bandarini hapo. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (katikati), akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), wakati wa ziara ya kikazi katika Bandari ya Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko. Kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Freddy Liundi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

No comments

Powered by Blogger.