Sugu aonyesha mjengo wa hoteli yake iliyokamilika

Mbunge wa Mbeya mjini, Mhe. Joseph Mbilinyi (Sugu) ameonyesha hoteli yake iliyokamilika ambayo ipo jijini Mbeya inaitwa Desderia aliyoanza kuijenga mwaka 2016.
Hata hivyo kipindi cha nyuma Mhe. Mbilinyi aliwahi kuposti picha ya ujenzi wa hoteli hiyo katika ukurasa wake wa instagram kuandika: Mkurugenzi wa Hotel Desderia Co Ltd Mr Joseph Mbilinyi na Eng. Chao Nan wa kampuni ya ukandarasi Home Africa Investment Co Ltd ya China wakisaini mkataba wa ujenzi. Kampuni hiyo itajenga hotel ya nyota 3 itakayoitwa Hotel Desderia jijini Mbeya na ujenzi unaanza mara moja kwa mkopo wa bank ya CRDB.

No comments

Powered by Blogger.