VIGOGO WENGINE WAWILI WACHUKUA FOMU KUWANIA URAIS TFF, YUMO MWAKALEBELA

Idadi ya wanaowania nafasi ya urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeendelea kuongezeka ambapo sasa kuna mgombea mwingine amechukua fomu.
Frederick Mwakalebela, kigogo wa zamani wa shirikisho hilo, amechukua fomu ya kuwania urais katika ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam, leo Jumapili, huku pia Athumani Nyamlani ambaye katika uchaguzi uliopita alishiriki lakini kura hazikutosha, naye amerejea kwa mara nyingine kuchukua fomu ya kuwania urais.

Wengine ambao tayari wameshachukua fomu za kuwania urais ni:
Jamal Malinzi
Imani Madega
Wallace Karia
Fredrick Masolwa

Wanaowania nafasi ya MAKAMU RAIS hadi sasa ni;
Mulamu Nghambi
Michael Wambura
Geofrey Nyange

No comments

Powered by Blogger.