Mbowe ajibu tuhuma za dawa za kulevya

                                              Mkutano wa Freeman Mbowe na wanahabari

Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amekanusha tuhuma za kuhusika na dawa za kulevya ikiwa ni siku chache baada ya kutajwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika orodha ya watu 65 wanadaiwa kuhusika na dawa za kulevya.
Akizungumza na wanahabari leo Mjini Dodoma Mbowe amesema hajawahi kujihusisha kwa kufanya biashara wala kutumia madawa ya kulevya wakati wote katika maisha yake.
Pia Mbowe amesema kuwa vita hiyo imechelewa sana kuanza kwani ilipaswa kuanza miaka mingi iliyopia, kwa kuwa imekuwa ikididimiza mandeleo ya Taifa.
Mbowe amesema kuwa CHADEMA inaunga mkono vita dhidi ya dawa za kulevya na iko tayari kuungana na yeyote atakayeiendesha bila kujali, lakini haiko tayari kuunga mkono vita yenye ila ndani yake.

No comments

Powered by Blogger.