Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums Maxence Melo Aachiwa kwa dhamana

Mwanzilishi wa mtandao wa JamiiForums  Maxence Melo   ameachiwa kwa dhamana leo  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, baada ya kukaa mahabusu kwa takribani siku 5.

Melo anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).

Mashtaka mengine ni kuzuia na kuharibu taarifa ambazo Jeshi la Polisi wamekuwa wakizitaka kwa ajili ya uchunguzi chini ya kifungu cha 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao na kushindwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi  na kuharibu uchunguzi chini ya kifungu cha namba 22 cha Sheria ya Makosa ya Mitandao.

No comments

Powered by Blogger.