MANCHESTER CITY YAKWEA HADI KATIKA NAFASI YA PILI KATIKA LIGI KUU YA UINGEREZA

Timu ya Manchester City imekwea hadi nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Hull City wakiwa ugenini katika dimba la KCOM.

Kikosi cha Pep Guardiola kilipata ushindi wake wa 12 katika msimu huu, na kuwa nyuma kwa pointi saba dhidi ya vinara timu ya Chelsea.

Yaya Toure alifunga goli la kwanza kwa mkwju wa penati katika kipindi cha pili, baada ya Raheem Sterling kuchezewa rafu, Kelechi Iheanacho akafunga la pili na Curtis Davies kujifunga la tatu.

                                  Yaya Toure akifunga goli kwa mkwaju wa penati
                       Kelechi Iheanacho akifunga goli la pili la Manchester City
  Curtis Davies akijifunga wakati akijaribu kuokoa mpira uliopigwa na Raheem Sterling

No comments

Powered by Blogger.