Milionea Anayelipa Bilioni 20 kwa Ajili ya Plate Number ya Gari

 MILIONEA mmoja raia wa India, Balwinder Sahni huilipa Serikali ya Dubai dola milioni 9 sawa na Tsh. Bilioni 19.617 kila mwaka kwa ajili ya kulipia leseni ya  Plate Number (special number) ya gari lake ambalo lina namba moja tu.
 Balwinder Sahni ambaye anafanya biashara zake nchini Dubai hutumia gharama hiyo kulipia ili aendelee kuimiliki plate number ya moja ya magari yake 6 aina ya Rolls Royce.
 Balwinder Sahni, ambaye anamiliki mali nyingi mjini humo ameiambia CNN kuwa, anaipenda sana plate number yake hiyokwani inamsaidia kumtangaza hivyo kumrahisishia na kumuongezea watu wengi ambao humtafuta ili kufanya naye biashara.
 Pia husikitishwa na watu wanaomshutumu kuwa anatumia pesa zake vibaya.
“Ni vigumu, watu wanasema bila kufahamu mimi ni nani. Mimi ni mtu wa kawaida tu.” Sahni aliiambia CNN Money.

No comments

Powered by Blogger.