LIVERPOOL YAFANYA KUFURU NA KUKWEA KILELENI MWA LIGI KUU YA UINGEREZA

Liverpool imekwea kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza kwa mara ya kwanza ikinolewa na kocha Jurgen Klopp kwa kupata ushindi mnono wa magoli 6-1 dhidi ya Watford katika dimba la Anfield.

Sadio Mane aliifanya Liverpool iongoze kwa kufunga kwa mpira wa kichwa cha sarakasi, baada ya wenyeji hao kukosa nafasi kadhaa, na kisha baadaye Philippe Coutinho kufunga la pili kwa shuti la umbali wa yadi 20.

Adam Lallana alimdondoshea krosi Emre Can na kufunga goli la tatu kabla ya mapumziko. Kipindi cha pili kilipoanza Roberto Firmino aliunganisha kimiani pande la Lallana kabla ya Mbrazili huyo kumtengenezea goli Mane na kisha Georginio Wijnaldum kutikisa la sita.
 Msenegal Sadio Mane akiruka kichwa cha sarakasi na kufunga goli la kwanza
          Roberto Firmino akiifungia Liverpool goli la nne katika mchezo huo
 Sadio Mane akifunga goli lake la pili katika mchezo huo ambalo lilifikisha idadi ya magoli matano ya Liverpool

No comments

Powered by Blogger.