THEO WALCOTT AENDELEZA MAKALI YAKE KATIKA LIGI KUU YA UINGEREZA

 Baada ya kushindwa kufanya vyema na timu ya taifa ya Uingereza, Theo Walcott ameendeleza makali yake akiwa na Arsenal na kuisaidia kuibuka na ushindi wa magoli 3-2 dhidi ya Swansea katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Mshambuliaji huyo wa Arsenal na Uingereza sasa ana magoli matano katika michezo minane, alifunga goli la kwanza kufuatia makosa ya Jordi Amat na kisha kuongeza la pili kupitia mpira wa kichwa uliopigwa vibaya na Jack Cork.

Swansea wakiwa na kocha wao mpya Bob Brandley walionekana kupoteza matumaini baada ya magoli hayo, hadi pale Gylfi Sigurdsson alipofunga goli kufuatia makosa yaliyofanywa na Granit Xhaka na kuwapa matumaini.

Mesut Ozil aliifungia Arsenal goli la tatu kufuatia krosi iliyopigwa na Alexis Sanchez, hata hivyo mchezaji aliyetokea benchi Borja Baston aliiunganisha wavuni krosi iliyopigwa kiufundi na Modou Barrow na kufunga goli la pili.
  Theo Walcott akishangilia goli lake la kwanza alilolifunga katika mchezo huo
   Borja Baston akifunga goli la pili la Swansea na kuipa presha Arsenal

No comments

Powered by Blogger.