CHURA WA SNURA AFUNGULIWA.

 Msanii Snura Mushi 'Snura'akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutambulisha Video yake ya wimbo wa  chura mara baada ya kufunguliwa wimbo huo kupigwa na kuoneshwa kwenye vituo vya Luninga pamoja na wimbo wa chura kuanza kupigwa katika vituo vya Redio hapa nchini.
 Msemaji wa 'Snura', kulia akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar e Salaam leo mara baada ya kukamilisha video mpya ya wimbo wa chura wa Snura na wimbo huo kuanza kuchezwa kwenye vyombo mbalimbali vya Luninga pamoja na wimbo wa chura kuaza kupigwa kwenye vituo vya Redio.

Picha na Aviala Kakingo, Globu ya Jamii.
VIDEO mpya ya wimbo wa Msanii, Snura Mushi 'Snura' wa Chura ambao ulikuwa umefungiwa na Serikali, wimbo  huo umefunguliwa na kuanza kuchezwa na kuoneshwa kwenye vituo vya Luninga pamoja na kupigwa kwenye vituo vya Redio.
Hayo yamesemwa na Msanii, Snura Mushi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa wimbo huo ameurekodia Video mpya yenye maadili ya Kitanzania na yenye staa zote na inaelezea maana halisi ya chura kama alivyomaanisha kwenye utunzi wa wimbo huo.

No comments

Powered by Blogger.