BONDIA WA UZITO WA JUU TYSON FURY AKIRI KUBWIA UNGA AINA YA COCAINE

 Bondia Tyson Fury amekiri kutumia dawa za kulevya aina ya cocaine katika mahojiano marefu, ambayo yamebainisha hali ya afya ya akili yake aliyokuwa nayo hivi sasa, huku akisema kuwa kila siku anatarajia kufa.

Bondia huyo mwenye miaka 28 anahofia mabadiliko yake ya tabia, ambapo hivi jumatatu aliandika kuhusu kustaafu ngumi kwa kutumia akaunti yake ya twitta, na kisha baadaye kuandika kuwa ulikuwa ni uongo.

Jumbe zake hizo katika mitandao ya jamii zilifuatia uamuzi wa kujitoa kupigana Oktoba 29 kuwania mkanda wa ubingwa wa dunia dhidi ya Wladimir Klitschko, ambalo liliharishwa baada kuelezwa kuwa hayupo fiti kiafya.
Tyson Fury amekuwa akikabiliana na tatizo la msongo wa mawazo kwa muda sasa

No comments

Powered by Blogger.