JOSE MOURINHO ASIFIA GOLI TAMU LA HENRIKH MKHITARYAN

 Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amepongeza goli zuri lililofungwa kwa mpira wa kisigino kwa nyuma na Henrikh Mkhitaryan katika mchezo walioibuka na ushindi dhidi ya Sunderland katika dimba la Old Trafford.

Mkhitaryan alifunga goli hilo lililozua utata kutokana na kuwa alikuwa ameotea akipokea pasi kutoka kwa Zlatan Ibrahimovic na kufanya matokeo ya mchezo huo kuwa Manchester 3-1 Sunderland.

Mkhitaryan mwenyewe amesema goli hilo ni goli zuri kuwahi kufunga katika maisha yake ya soko, na kuongeza kuwa hayo yalikuwa ni mazingaumbwe madogo ya kipindi cha Sikukuu ya Krismasi.

No comments

Powered by Blogger.