Wazungu Waliomtia Mtu Mweusi Kwenye Jeneza Akiwa Hai Washtakiwa
Mtu
mweusi nchini Afrika Kusini ambaye alidaiwa kulazimishwa kuingia katika
jeneza na wakulima wawili weupe kwa kupita katika shamba lao amesema
kuwa anahofia maisha yake.
Victor Mlotshwa alikuwa akizungumza nje
ya mahakama ya mji wa kaskazini mashariki wa Middelburg ambapo waliotaka
kumshambulia waliwasilishwa katika mahakama.
”Nilidhani wataniua”,alisema.
Kanda ya video ya dakika 20 iliorekodi kisa hicho imekuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini.
Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani huko
Middelburg anasema kuwa ndani ya mahakama hiyo ,washtakiwa hao ,Theo
Martins Kackson na Willem Oosthuizen,walisimama wakiwa wameinamisha
vichwa vyao chini huku waandishi wa habari na raia wakichukua picha zao.
”Nilidhani wataniua”,alisema.
Kanda ya video ya dakika 20 iliorekodi kisa hicho imekuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini.
Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani huko
Middelburg anasema kuwa ndani ya mahakama hiyo ,washtakiwa hao ,Theo
Martins Kackson na Willem Oosthuizen,walisimama wakiwa wameinamisha
vichwa vyao chini huku waandishi wa habari na raia wakichukua picha zao.
Wameshtakiwa kwa kumteka nyara na kumshambulia kwa lengo kumjeruhi vibaya.Hawajakubali ama kukana mashtaka hayo.
Wawili hao wanazuiliwa hadi tarehe 25
Januari huku waendesha mashtaka wakisema kwamba walihitaji muda zaidi
kuchunguza ,ikiwemo kuthibitisha video hiyo.
Mamake bw Mlotshwa alijawa na hasira na
kushindwa kujizuia wakati wa kusikizwa kwa kwesi hiyo.Nje ya mahakama
kulikuwa na kelele za wafuasi wa vyama vikuu nchini humo huku
#RacismMustFall ikisambazwa katika mitandao ya kijamii.
Post a Comment