MUONEKANO WA NDEGE YA AIR FORCE ONE

SIFA KUBWA:
Ndani ya ndege hiyo kuna ofisi ya rais, jiko, chumba cha mikutano, bafu, sehemu ya kuvalia nguo, eneo la kufanyia mazoezi ‘gym’ na chumba cha mawasiliano. Ndiyo maana inasemwa ni nyumba inayotembea.

Pia kuna chumba cha maafisa wanaomlinda rais, sehemu yao ya kufanyia mkutano wakipata dharura na zahanati kama rais akiugua ghafla wakati ndege ipo angani.
Si hayo tu, kuna chumba chenye simu 85 za mezani na Tivii 19 kwa ajili ya kupata habari za kidunia wakati ndege ipo juu.
Ndege hiyo haikamiliki kuiita Air Force One bila kutambulisha sehemu maalum ambayo hutumika kijeshi kumkwepesha adui anayetaka kuilenga kwa lengo la kuilipua.


No comments

Powered by Blogger.